Eto’o kulamba mwaka mmoja Anfield

kwa ufupi
Eto’o kwa sasa ni mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake na klabu ya Chelsea na hivyo Liverpool wanataka kumpa mwaka mmoja wa kuichezea timu yao licha ya sasa kuwa kwenye hatua nzuri ya kumsainisha Mario Balotelli

SUPASTAA wa Cameroon, Samuel Eto’o amepewa ofa ya mkataba wa mwaka mmoja kujiunga na klabu ya Liverpool kwa ajili ya mikikimikiki ya Ligi Kuu England na Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu huu.
Eto’o kwa sasa ni mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake na klabu ya Chelsea na hivyo Liverpool wanataka kumpa mwaka mmoja wa kuichezea timu yao licha ya sasa kuwa kwenye hatua nzuri ya kumsainisha Mario Balotelli.
Wakala wa Eto’o amekuwa akiwasiliana na klabu mbalimbali kwenye majira ya haya ya kiangazi kwa ajili ya mteja wake apate timu ya kucheza kufuatia kutemwa na Chelsea.
Imeripotiwa kwamba staa huyo wa Cameroon anataka kubaki kwenye Ligi Kuu England na hivyo kupata ofa hiyo ya mwaka mmoja Anfield ni jambo kubwa kwake.
Liverpool imepanga kumpa Eto’o mshahara wa Euro 93,000 kwa wiki na bonasi nyingine zitakazotokana na kiwango chake cha uwanjani.    

Related Posts:

  • Eto’o kulamba mwaka mmoja Anfieldkwa ufupi Eto’o kwa sasa ni mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake na klabu ya Chelsea na hivyo Liverpool wanataka kumpa mwaka mmoja wa kuichezea timu yao licha ya sasa kuwa kwenye hatua nzuri ya kumsainisha Mario Balot… Read More
  • Mario Balotelli kwenda liverpool Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers anataka kumsajili mshambuliaji wa AC Milan Mario Balotelli, huku pauni milioni 14 ikidhaniwa kutosha kufanikisha uhamisho wake (Sunday Express),… Read More
  • Panga pangua, hii ndio Yanga mpya IN SUMMARY Kwa mujibu wa mazoezi yaliyofanyika Dar es Salaam na hapa Pemba jumlisha na mechi ya kirafiki waliyocheza, ‘First Eleven’ ya Yanga itakuwa kama ifuatavyo; HII ni siri usimwambie mtu yeyote, uchune nayo hi… Read More
  • matokeo ya mechi za premier league Aston Villa 0 - 0 Newcastle United Southampton 0 - 0 West Bromwich Albion Chelsea 2 - 0 Leicester City half-time: (0 - 0) match details : 63'Diego Costa 1, 77'Eden Hazard 2 Crystal Palace 1 - 3 West Ham United half-time: (… Read More
  • WENGER ASEMA MILANGO IPO WAZI KWA THOMAS VERMAELEN Kocha wa Arsenal , Arsene Wenger amethibitisha kwamba beki wake wa kati Thomas Vermaelen ambaye amebakisha mwaka mmoja katika mkataba wake huenda akaiama club hiyo maarufu kama wabeba mitutu wa london katika kipindi hiki cha… Read More