Malori yote ya msafara wa misaada kutoka Urusi ambayo yalisafiri bila idhini hadi katika eneo linalodhibitiwa na waasi mashariki mwa Ukraine siku ya ijumaa yamerudi nchini Urusi.


Afisa mmoja wa forodha amesema kuwa malori kadhaa yalikaguliwa na kurudi nchini Urusi.
Zaidi ya malori mia mbili ya misaada yalisafiri hadi katika mji wa Luhansk siku ya ijumaa,baada ya Urusi kusema kuwa imechoka kungojea idhini kutoka kwa serikali ya Ukraine.
Urusi inasema kuwa msaada huo ulikuwa wa kibinaadamu,lakini mataifa ya Magharibi yanasema kuwa unatumiwa na Urusi kuvamia Ukraine.

Malori ya misaada ya Urusi


Kansela wa Ujerumani Angela Merkel anatarajiwa kufanya mazungumzo mjini Kiev na rais wa Ukraine Petro Poroshenko pamoja na waziri mkuu Arseniy Yatsenyuk.

Related Posts:

  • Kijiji chafunikwa na maporomoko,India Zaidi ya watu 200 wanahofiwa kukwama katika maporomoko ya udongo nchini India,huku 20 wakithibitishwa kufariki dunia katika kijiji cha kijiji cha Malin karibu na mji wa Pune lilikotokea janga hilo. Kazi ya uokoaji inaend… Read More
  • Raisi Barack OBama kufikishwa mahakamani Atashtakiwa kwa kosa la matumizi mabovu ya madaraka chanzo: http://www.usatoday.com/story/news/politics/2014/07/29/president-obama-appeals-court-health-care-law/13316989/ … Read More
  • Tetemeko la ardhi China laua 380 Wafanyakazi wa Uokoaji nchini China wanaendelea kujitahidi kufikia eneo la lilipigwa na tetemeko la ardhi katika jimbo la Yunnan siku ya jumapili na kuua watu zaidi ya mia tatu na themanini. Kikosi cha dharura kinajaribu ku… Read More
  • Polisi akamatwa kwa wizi wa Cocaine Polisi wa Ufaransa wamemkamata afisa mmoja wa kukabiliana na mihadarati kwa kuiba kilo hamsini za Cocaine kutoka makao makuu ya polisi mjini Paris. Dawa hiyo yenye thamani ya dola millioni 4 ilikuwa imefungiwa katika chumba… Read More
  • Ebola:Shule zote zafungwa Liberia Rais wa Liberia,Ellen Johson Sirleaf ametangaza amri ya kufungwa kwa shule zote nchini humo kama mpango wa taifa hilo wa kukabiliana na ugonjwa wa homa ya Ebola. Mpango huo pia unashirikisha kuzitenga baadhi ya jamii zil… Read More