Mateka waendeshwa kwata Ukraine

Wapiganaji wa mashariki mwa Ukraine wanaoipendelea Urusi wamewaendesha kwata katika barabara za mji wa Donetsk, wanajeshi kadha wa Ukraine waliowateka.
Donetsk ni ngome ya wapiganaji hao.
Wafungwa wakipitishwa barabara za Donetsk siku ya kuadhimisha uhuru wa Ukrainee
Mambo hayo yamejiri siku ya kuadhimisha uhuru wa Ukraine.Watu waliosimama kando ya barabara waliwazomea "mafashisti" wafungwa hao walioonekana wachafu.
Katika kuadhimisha siku hiyo Rais wa Ukraine, Petro Poroshenko, aliahidi kutumia dola bilioni 3 kulipatia jeshi zana mpya katika miaka mitatu ijayo.
Akitoa hotuba kwenye gwaride katika mji mkuu, Kiev, Rais Poroshenko alisema Ukraine imekuwa ikipigana vita hasa dhidi ya uvamizi wa kigeni, na Ukraine itakabili tishio la kijeshi kila mara katika siku za usoni:
"Kufuatana na mpango wa mwaka 2015-17 dola bilioni 3 zitatumiwa kununua silaha na zana mpya za kijeshi.
Hiyo itawezesha kukarabati, kununua na kulipatia jeshi ndege, helikopta, manuwari na mashua.
Huu ndio mwanzo tu."

Related Posts:

  • Kobe aliyepotea akamatwa na polisi huo Los Angeles ALHAMBRA, Calif. (AP) -- At least officers didn't have to cite it for speeding when the Alhambra Police Department pulled over a giant tortoise found wandering on a local street. Police say the hard-shelled reptile was nab… Read More
  • Ebola:Shule zote zafungwa Liberia Rais wa Liberia,Ellen Johson Sirleaf ametangaza amri ya kufungwa kwa shule zote nchini humo kama mpango wa taifa hilo wa kukabiliana na ugonjwa wa homa ya Ebola. Mpango huo pia unashirikisha kuzitenga baadhi ya jamii zil… Read More
  • Kijiji chafunikwa na maporomoko,India Zaidi ya watu 200 wanahofiwa kukwama katika maporomoko ya udongo nchini India,huku 20 wakithibitishwa kufariki dunia katika kijiji cha kijiji cha Malin karibu na mji wa Pune lilikotokea janga hilo. Kazi ya uokoaji inaend… Read More
  • Polisi akamatwa kwa wizi wa Cocaine Polisi wa Ufaransa wamemkamata afisa mmoja wa kukabiliana na mihadarati kwa kuiba kilo hamsini za Cocaine kutoka makao makuu ya polisi mjini Paris. Dawa hiyo yenye thamani ya dola millioni 4 ilikuwa imefungiwa katika chumba… Read More
  • Tetemeko la ardhi China laua 380 Wafanyakazi wa Uokoaji nchini China wanaendelea kujitahidi kufikia eneo la lilipigwa na tetemeko la ardhi katika jimbo la Yunnan siku ya jumapili na kuua watu zaidi ya mia tatu na themanini. Kikosi cha dharura kinajaribu ku… Read More